Ninaiheshimu na kuitamani sana imani ya Ibrahimu kama inavyoonyeshwa katika Biblia. Tunapoiangalia imani ya Ibrahimu, tunaweza kuona mateso na juhudi ya imani yake ambayo kwa hiyo alimfuata Yehova, na kwa jinsi hiyo hatuwezi kufanya lolote bali ni kuitamani imani ya Ibrahimu. Mungu alimbariki sana Ibrahimu, kama inavyoonyeshwa katika Mwanzo 12:3, ambapo Mungu alisema, “Nitawabariki wote watakaokubariki, Na nitamlaani yeyote atakayekulaani; na katika wewe jamaa wote wa dunia watabarikiwa.” Baraka hizi nyingi zinaonekana pia katika Mwanzo 15:1, ambapo Mungu alitamka kwa Ibrahimu kuwa “Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana”. Mungu alikuwa na upendo maalum kwa Ibrahimu kiasi kwamba Mungu alijiona kuwa ni Mungu wa Ibrahimu.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Isaya alikuwa ni nabii aliyeishi karibu miaka 700 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo hapa duniani. Pamoja na kuwa alitangulia kabla ya kuja kwa...
Katika sura ya 17 ya kitabu cha Mwanzo, agano la tohara ambalo Mungu amelianzisha na kulithibitisha na Ibrahimu linatuonyesha sisi juu ya tohara ya...
Hebu tuanze kwa kuangalia Kutoka 3:13-16: “Musa akamwambia Mungu, ‘Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli na kuwaambia, ‘Mungu wa baba zenu amenituma kwenu,’ nao...