Katika sura ya 17 ya kitabu cha Mwanzo, agano la tohara ambalo Mungu amelianzisha na kulithibitisha na Ibrahimu linatuonyesha sisi juu ya tohara ya kiroho ambayo kwa hilo dhambi zote zinaondolewa toka kwa waisraeli kwa kuiweka mikono yao juu ya mwanasadaka wa kuteketezwa katika Hema Takatifu la Kukutania na kwa jinsi hiyo walizipitisha dhambi zao kwa mnyama huyo wa sadaka ya kuteketezwa. Kwa maneno mengine, agano ambalo Mungu alilolianzisha na kulithibitisha na Ibrahimu lilikuwa ni wonyesho unaoonyesha juu ya sadaka ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa zitakazokuja baadaye. Ahadi ambayo Mungu aliifanya kwa Ibrahimu kwa tohara, kwamba atakuwa Mungu wake na Mungu wa wazawa wake, ilitabiri hali ikiliheshimu Hema Takatifu la Kukutania, kwamba wazawa wa Ibrahimu watazipitisha dhambi zao katika sadaka ya kuteketezwa kwa kuiweka mikono yao juu ya kichwa cha mwanasadaka. Ni lazima tutambue na tuamini kuwa hii inatuonyesha sisi kwa nyongeza kwamba katika kipindi cha Agano Jipya Yesu atazichukua dhambi zote za ulimwengu kwa ubatizo wake alioupokea toka kwa Yohana.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Kuna tofauti za wazi kati ya imani ya wale waliozaliwa upya na ile ya wakristo wa mazoea: imani ya wale waliozaliwa upya inafahamu na...
Mungu alimwamuru Musa kwenda juu katika Mlima Sinai na akampatia mtitiriko mzima wa Sheria yake. Kwanza kabisa, alimpatia Musa Amri Kumi: “Usiwe na miungu...
Uzio wa ua wa mstatiri wa Hema Takatifu la Kukutania ulikuwa na kipimo cha dhiraa 100 kwa urefu. Katika Biblia, dhiraa ilihesabiwa kutokana na...