Kuna tofauti za wazi kati ya imani ya wale waliozaliwa upya na ile ya wakristo wa mazoea: imani ya wale waliozaliwa upya inafahamu na kuamini kuwa Mungu amezifuta dhambi zao zote, na imani ya wakristo wa mazoea inamwamini Yesu kwa kuyategemea mawazo yao binafsi, ni kama suala la kidini tu. Pamoja na hayo wale wanaomwamini Mungu kama sehemu ya masuala ya kidini wanafanikiwa sana kiasi kuwa wale wanaohubiri ukweli halisi wanaumizwa moyo pale wanapowaona watu hawa wenye imani potofu wakiyaeneza mafundisho yao ya uongo huku wakifanikiwa. Wanaumizwa mioyo kwa sababu wanafahamu wazi kuwa Wakristo wengi sana wanaletwa katika dini hiyo ya uongo na udanganyifu.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Isaya alikuwa ni nabii aliyeishi karibu miaka 700 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo hapa duniani. Pamoja na kuwa alitangulia kabla ya kuja kwa...
Mungu alimwamuru Musa kwenda juu katika Mlima Sinai na akampatia mtitiriko mzima wa Sheria yake. Kwanza kabisa, alimpatia Musa Amri Kumi: “Usiwe na miungu...
Uzio wa ua wa mstatiri wa Hema Takatifu la Kukutania ulikuwa na kipimo cha dhiraa 100 kwa urefu. Katika Biblia, dhiraa ilihesabiwa kutokana na...